Sale
47324_Mabandia-COVER_0

Mabandia

0 customer reviews

Original price was: KSh 500.00.Current price is: KSh 435.00.

Compare
Category:
Mabandia
Original price was: KSh 500.00.Current price is: KSh 435.00.

‘Mabandia’ ni tamthilia inayopiga kurunzi ubandia unaojificha na kujifichua kwa sura mbalimbali maishani. Maisha ni kama karata. Wahusika sita wanajitokeza katika maonyesho sita wakifululiza hadi barazani kucheza duru sita za mchezo maarufu wa Wahedi wa Sitini. Mchezo huu huchezwa hasa katika maeneo ya pwani ya Afrika Mashariki.

Kupitia vitendawili vinavyoibuka katika maonyesho mbalimbali, mwandishi anagubika hoja kadhaa za ubandia. Hoja hizi zinalenga kutafakarisha jinsi ubandia huo unavyoathiri mitazamo ya binadamu katika nyanja mbalimbali za maisha.

Ali Attas ni mwandishi mtajika wa vitabu kadhaa vikiwemo kamusi, vitabu vya lugha na vilevile vya hadithi. Kama mhariri wa vitabu vya elimu, mtangazaji, mwandishi habari na mwalimu wa lugha na fasihi mwenye uzoefu mkubwa, amebugia tajriba pana na za kipekee katika ukumbi wa kukikuza Kiswahili.

Reviews

0
0 customer reviews
5
0
4
0
3
0
2
0
1
0

There are no reviews yet.

Be the first to review “Mabandia”

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Select at least 2 products
to compare